Psalms 16:1-6
Sala Ya Matumaini
(Utenzi wa Daudi)
1 aEe Mungu, uniweke salama,
kwa maana kwako nimekimbilia.
2 bNilimwambia Bwana, “Wewe ndiwe Bwana wangu;
pasipo wewe sina jambo jema.”
3 cKwa habari ya watakatifu walioko duniani,
ndio walio wa fahari ambao ninapendezwa nao.
4 dHuzuni itaongezeka kwa wale
wanaokimbilia miungu mingine.
Sitazimimina sadaka zao za damu
au kutaja majina yao midomoni mwangu.
5 e Bwana umeniwekea fungu langu na kikombe changu;
umeyafanya mambo yangu yote yawe salama.
6 fAlama za mipaka zimeniangukia mahali pazuri,
hakika nimepata urithi mzuri.
Copyright information for
SwhKC