Psalms 16:1-6

Sala Ya Matumaini

(Utenzi wa Daudi)


1 aEe Mungu, uniweke salama,
kwa maana kwako nimekimbilia.


2 bNilimwambia Bwana, “Wewe ndiwe Bwana wangu;
pasipo wewe sina jambo jema.”

3 cKwa habari ya watakatifu walioko duniani,
ndio walio wa fahari ambao ninapendezwa nao.

4 dHuzuni itaongezeka kwa wale
wanaokimbilia miungu mingine.
Sitazimimina sadaka zao za damu
au kutaja majina yao midomoni mwangu.


5 e Bwana umeniwekea fungu langu na kikombe changu;
umeyafanya mambo yangu yote yawe salama.

6 fAlama za mipaka zimeniangukia mahali pazuri,
hakika nimepata urithi mzuri.

Copyright information for SwhKC